MAONI YA WADAU WA ELIMU YATHAMINIWE
Na
Kibindo,Zanialy
LICHA ya hatua tuliyopiga kwenye sekta ya elimu tangu uhuru wa nchi
yetu mwaka 1961ikiwemo ongezeko la shule pamoja na vyuo vya elimu, bado sekta hii
nyeti inakabiliwa na changamo nyingi hali inayosababisha kudhoofu kwa hali ya
elimu nchini.
Kwa
kutambua umuhimu wa sekta hii nyeti ya elimu wadau wa elimu wanafanya jitihada mbalimbali kuinusuru sekta hii ,makala hii inatazama
moja ya kongamano lililoandaliwa na shirika la HakiElimu kwa kushirikiana na
Umoja wa walimu wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSTA).
Kongamano
hilo lilifanyika mnamo tarehe 26 Novemba mwaka kwa lengo la kutathmini hali ya
elimu nchini; miaka 50 tangu uhuru wa Tanzania Bara mwaka 1961.
Hata
hivyo pamoja na mafanikio yaliopongezwa na kongamano hilo changamoto mbalimbali
zinazoikabili sekta ya elimu zilibainika,
changamoto hizo ni pamoja na ongezeko la idadi ya wanafunzi wanaoshindwa
mitihani, na kuporomoka kwa ubora wa elimu,mfano uwepo wa watoto
wanaohitimu darasa la saba bila kujua kusoma na kuandika.
Aidha,
uhaba mkubwa wa miundombinu ya
kujifunzia na kufundishia pamoja na ukosefu wa walimu bora ambao ni muhimu kwa
utoaji wa elimu bora bado ni tatizo kubwa.
Changamoto
nyingine ni maslahi mabovu ya walimu na watumishi wa ngazi za kawaida
mashuleni.
Aliyewahi
kuwa Waziri wa Elimu katika serikali ya kwanza, Jackson Makwetta alisema
kuporomoka kwa elimu nchini kunatokana na uwepo na viongozi wababaishaji,
wasemaji wa maneno mengi bila utekelezaji na kukosa ufuatiliaji.
Kwa
upande wake Dk. Kitila Mkumbo alisema
kuwa, kwa sasa taifa lazima liamue kukubaliana na maoni ya wataalamu kuhusu
lugha ya kufundishia kama iwe ni Kiswahili, hali aliyosema itawasaidia
wanafunzi kuelewa vyema wanachofundishwa darasani,Kama sivyo basi Kiingereza
kifundishwe vizuri ili wanafunzi wakielewe na waweze kukitumia ipasavyo.
Kilichosisistizwa
na watoa mada na washiriki wa Kongamano hilo ni kuwa, pamoja na kwamba
tunastahili kujivunia mafanikio tuliyofikia tangu uhuru lakini ifikie mahala
watoto wetu wanapata elimu bora ili waweze kukabiliana na changamoto
zinazowazunguka pamoja na jamii zao.
Imefika
wakati badala ya kuendelea kujenga shule mpya, pengine sasa tuangalie
zaidi namna ya kuboresha ufundishaji,ufundishwaji pamoja na vitendea kazi
kwenye shule zilizopo ili wanafunzi wapate ujuzi wanaohitaji sasa na baadaye
katika maisha yao.
Ujuzi
au uwezo huo ni pamoja na ule utakaomuwezesha mwanafunzi kujiamini na kujituma,
kuweza kutatua matatizo na kukabiliana na changamoto kwa ufanisi na kuchambua
na kutathmini taarifa kwa ufasaha na umakini zaidi.
Elimu
yetu inapaswa iwape wanafunzi uwezo wa kutumia mitazamo waliyojifunza kwenye
eneo moja katika maeneo mengine pamoja na kuwapa uwezo wa kuelewa na kuwa
tayari kuchangia mahitaji ya jamii zao na taifa kwa ujumla.
Dk.
Hillary Dachi yeye alizungumzia zaidi kuporomoka kwa hadhi ya ualimu tangu nchi
ilipopata uhuru kiasi kwamba sasa hivi walimu wanaishi maisha ya dhiki na wengi
hawaipendi kazi hiyo.
Ualimu
umepoteza hadhi na heshima yake katika jamii,ni kazi ambayo kwa vijana wengi ni
chaguo lao la mwisho,mfano imezoeleka sana nchini kwa mtoto asipo-fanya vizuri
(akifeli) akapata madaraja ya chini sana anatafutiwa kozi ya ualimu.
Walio
wengi, taaluma ya ualimu ni kama suluhisho la maisha kwamba unapokosa kila
kitu, anakuwa huna jinsi ila ni kukimbilia kujifunza ualimu.
Na
kwa sababu ukiwa katika ualimu ni rahisi sana kujiendeleza, kwa hiyo walio
wengi wanabadilisha taaluma wanaenda katika taaluma nyingine.
Hali
hii inasababisha ugumu wa kupata walimu wa kutosheleza kwa sababu hakuna namna
yeyote tunayoifanya kama serikali kuhakikisha kwamba walimu wanaipenda kazi
yao, wanaendelea kufundisha na wanapenda kufahamika kama walimu.
Dk.
Dachi alitoa angalizo kuwa taifa halitapata walimu wa kutosha ikiwa hakuna
juhudi za makusudi za kumfanya mwalimu aliyepo aendelee kufanya kazi yake kwa
moyo mmoja na kwa kujituma.
Kukosekana
kwa Bodi ya taaluma ya ualimu ambayo ingeweza kusajili walimu na kusimamia
maadili na mambo mengine yanayohusiana na taaluma ya ualimu pia imebaki kuwa
changamoto kubwa.
Maoni kama haya ya wadau wa
elimu ni vyema yakapewa nafasi stahiki ili kulinusuru sekta hii muhimu kwa
mustakabali wa maendeleo ya Taifa letu.
Aidha
wenye dhamana ya kusimamia elimu nchini,wadau wa elimu na watanzania kwa ujumla
ni sharti tushikamane na kila mmoja kuwajibika katika nafasi yake ili kuinusuru
elimu yetu kwa mustakabali wa vizazi vyetu naTaifa kwa ujumla.
0764-784649
zankibindo@gmail.com
0 comments:
Post a Comment