HABARI
ZA MITANDAONI ZISIWEKE MAISHA YA WATANZANIA REHANI
Habari
mitandaoni kupitia blogs,a mitadao ya kijamii zimekuwa mkombozi vyanzo muhimu
vya habari kutokana na ufanisi na uwezo wake wa kufikisha habari toka sehemu
mbalimbali za Tanzania na nje ya Tanzania kwa haraka na muda muafaka uwezo
ambao vyombo vya habari kama Radio,Televisheni pamoja na magazeti havina.
Aidha
vyombo hivi vimekuwa mkombozi kutokana na kukosekana kwa sheria ya moja kwa kwa
moja ya kuvibana vyanzo hivi vya habari kama ilivyo kwa sheria za magazeti na
vyombo vya utangazaji yaani Radio na Televisheni hali inayovipa nafasi vyanzo
hivi vya habari kuwa huru katika utoaji wa habari ambazo Radio na Televisheni
na magazeti zisingeweza kutoa kwa kuofia
kwenda kinyume na sharia zinazoogoza vyombo hivyo.
Uhuru
huu wa habari za mitandaoni wakati mwingine umekuwa ukitumika vibaya na baadhi ya watu kwa
kuanzisha mitandao iliyojaa picha za ngono,stori za maisha ya watu ,video za
ngono huku mambo yenye tija kwa jamii
kama vile elimu ya kilimo bora,bei za bidhaa masokoni,taarifa za hali ya
hewa zinazohitajika na wakulima katika sughuli za kilimo zikinyimwa nafasi.
Dhana
ya habari kwamanufaa ya umma imepuuzwa kinachotazamwa sasa ni kipi kinapendwa
zaidi na jamii kwa lengo la kupata matangazo kutokana na kuwa na wafuatiliaji
wengi dhana hii haipaswi kuungwa mkono hata kidogo.Tusikubali mustakabari wa
maisha ya watazania yakachezewa na watu wachache kwa manufaa yao binafsi.
Imekuwa
ni kawaida sana kwa blog za watanzania kujaa story zinazohusu maisha binafsi ya
watu,picha za uchi,habari za chuki,kuchafuana,unafiki ili mradi mtu amejisikia
kuweka habari ianayomjia kichwani mwake bila kujali imani kubwa iliyopewa
mitandao hiyo.
Jambo
kubwa la kusikitisha mitandao hiyo yenye habari,picha na video chafu kuwa na
wapenzi wengi vijana wakiwa wengi zaidi,hali hii inasikitisha sana,wapi
tunalipeleka taifa hili,nini mustakabali wa maisha ya vijana wa
kitanzania,vizazi vya namna gani tunaviandaa.Sina lengo la kuunga mkono moja
kwa moja uthibiti wa matumizi ya mtandao lakini kwa hali hii ipo haja ya
udhibiti wa matumizi wa mitandao kwa manufaa ya umma.
Tumeziona
jitihada mbalimbali zilizofanywa na Tume ya udhibiti wa Mawasiliano Tanzania
(TCRA).Ikiwemo uendeshaji wa semina na warsha mbalimbali kwa wamiliki wa blog
lengo likiwa ni kusisitika matumizi sahihi ya mitandao kwa mustakabali wa
taifa.
Aidha
kampeni mbalimbali zinafanywa kusisitiza matumizi mzuri ya mitandao kukifuatiwa
na kauli mbiu mbalimbali kama vile ukiona ujumbe wa chuki,uchochezi na uongo
futa delete kabisa ili mradi tu kuhakikisha uhuru wa habari mitandaoni
unatumiwa vyema.
Licha
ya jitihada hizo bado tatizo la matumizi mabaya ya mitandao linashamiri
hususani uwepo wa picha zisizofaa mitandaoni,habari za uongo udaku ukitawala na
huku mambo ya msingi kwa maendeleo ya watu a taifa kwa ujumla kutopewa
kipaumbele.
Kwa
mantiki hii ipo haja sasa ya kusajili, kutoa mafunzo ya kimaadili na kitaaluma
kwa wamiliki wa blog nchini ili blogu hizo zilete mchago chanya kwa maendeleo
ya Taifa hili na si wao kuwa chanzo cha kuporomosha maadili ya vijana
wetu,kusababisha chuki na mengineyo mengi.
0 comments:
Post a Comment