PATA ELIMU HAPA

Kuharamisha Kuingilia Katika Tupu ya Nyuma
Allah (Subhaanahu wa Ta'ala) Amesema:
 “ Wake zenu ni konde zenu, basi ziendeeni konde zenu mpendavyo.” (Baqara: 223)
Ilikuwa ni tabia ya Mayahudi wakisema: Mtu atakapomuingilia mke wake mbele lakini kwa upande wa nyuma basi atazaliwa mtoto akiwa ni kengeza; ikashuka aya hii: Wake zenu ni mashamba yenu.” (Muslim). Katika riwaya nyingine:

 “…na ukipenda ufanye staili ya kama anasujudu na ukipenda sivyo hivyo yote ni sawa sawa...” (Muslim: Hadithi 1435)
Ilikuwa ni tabia ya ahlul kitaab kutomuingilia mwanamke ila kiubavu na katika hali ya mwanamke kujistiri. Na ilikuwa tabia ya baadhi ya Ansaar kuiga tabia zao hizo. Na wanaume wa ki-qureish walikuwa wamezowea kufanya mapenzi na wake zao vilivyo, wakistarehe nao kwa mbele, nyuma na kwa chali, (lakini bila ya kuwaingilia tupu zao za nyuma). Walipohamia Muhajirina Madina alioa mmoja wao mwanamke wa ki-ansaar; akataka kufanya nae mapenzi kwa mitindo waliyozoea (huko Makka) akachukizwa mwanamke yule na hilo, na akasema: Hakika sisi tulikuwa tukiingiliwa kiubavu, fanya hivyo au niepuke; kisa chao kikaenea, zikamfikia habari Mtume (Swalla Llaahu 'alayhi wa sallam) na Mwenyezi Mungu Akashusha:
14

 “Wake zenu ni konde zenu…” (Abu Daud)
Na Mtume (Swalla Llaahu 'alayhi wa sallam) akasema vile vile:
“(Waingilieni wake zenu kwa mtindo wa)Kwa mbele au (kwa mtindo wa) kwa nyuma lakini epukeni dubur (mkundu) na (kuwaingilia wakati wako) kwenye hedhi.” (Tirmidhi)

0 comments:

 
Top