Mr., kibindo |
Sekta ya elimu
nchini imejikuta kwenye wakati mgumu wa kudhoofika kwa hali ya elimu nchini
licha ya ongezeko kubwa la shule na vyuo
vya elimu ukilinganisha na kipindi cha uhuru miaka ya 1961 ambapo shule
zilikuwa chache lakini ufaulu ulikuwa mzuri ukilinganisha na ilivyo sasa.
Kufuatia hali
hii sekta ya elimu imejaribu kuja na mikakati tofauti ya kutatua tatizo hili
katika makala hii tutatazama mkakati uliozua maswali mengi uliotambulika kwa
lugha ya wenzetu kama “THE BIG RESULT NOW”yaani matokeo makubwa sasa.
Mkakati huo umelenga
kuongeza hali ufaulu kwa wanafunzi.Sina lengo la kuupinga moja kwa moja mkakati
huu kwa kuwa vipo vipengere muhimu kwa mtazamo wangu mfano matumizi ya alama
endelevu ambayo yatamsaidia manafunzi kupata alama anazostahili katika matokeo
ya mwisho.
Huwa Napata
shaka kama waliopewa dhamana ya kusimamia elimu hawafahamu chanzo halisi cha
matokeo mabaya au ndiyo siasa imewatawala?nisielekee huko sana ila mantiki
yangu hapa ni kujaribu kueleza matatizo yanayoitafuna sekta hii nyeti kwa
kupitia mitazamo mbalimbali ya wasomi pamoja na wadau wengine wa elimu.
Kwa kuanzia Mnamo
tarehe 26 Novemba mwaka 2011 shirika la HakiElimu kwa kushirikiana na Umoja wa
walimu wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSTA)waliandaa kongamano
lenye lengo la kutathmini hali ya elimu nchini; miaka 50 tangu Tanzania Bara
kupata uhuru wake mwaka 1961.
Kongamano hilo
liliithibitisha kwa takwimu ongezeko la idadi ya shule na vyuo, idadi ya uandikishwaji
na usawa baina ya wanafunzi wa kike na kiume. Kwa mfano lilisifu mafanikio
katika ongezeko la idadi ya shule za msingi kutoka shule 338 tu mwaka 1961 hadi
zaidi ya 15,000. Pia lilisifu ongezeko la idadi ya shule za sekondari kutoka 41
tu mwaka 1961 tu mwaka 1961 hadi 4,367 mwaka 2011.
Hata hivyo
pamoja na mafanikio hayo zilibainika changamoto mbalimbali ambazo zinaikabili
sekta ya elimu changamoto hizo ni pamoja na ongezeko la idadi ya wanafunzi
wanaoshindwa mitihani, na kuporomoka kwa
ubora wa elimu. Mfano uwepo wa watoto wanaohitimu darasa la saba bila kujua
kusoma na kuandika.
Aidha, kumekuwa na uhaba mkubwa wa miundombinu
ya kujifunzia na kufundishia pamoja na ukosefu wa waalimu bora ambao ni muhimu
kwa utoaji wa elimu bora.
Changamoto
nyingine ni maslahi mabovu ya walimu na watumishi wa ngazi za kawaida
mashuleni.
Aliyewahi kuwa
Waziri wa Elimu katika serikali ya kwanza, Jackson Makwetta alisema kuporomoka
kwa elimu nchini kunatokana na Tanzania kuwa na viongozi wababaishaji, wasemaji
wa maneno mengi, wasiotekeleza wanayoyasema na kukosa ufuatiliaji.
Naye Dk. Kitila
Mkumbo alisema kuwa, kwa sasa taifa lazima liamue kukubaliana na maoni ya
wataalamu kuhusu lugha ya kufundishia kama iwe ni Kiswahili, hali aliyosema
itawasaidia wanafunzi kuelewa vyema wanachofundishwa darasani.
Kama sivyo basi
Kiingereza kifundishwe vizuri ili wanafunzi wakielewe na waweze kukitumia
ipasavyo.
Kinachosisistizwa
na watoa mada na washiriki wa Kongamano hili ni kuwa, pamoja na kwamba
tunastahili kujivunia mafanikio tuliyofikia tangu uhuru lakini tufikie mahala
wanapata elimu bora ili waweze kukabiliana na changamoto zinazowazunguka pamoja
na jamii zao.
Imefika wakati badala ya kuendelea kujenga shule mpya,
pengine sasa tuangalie zaidi namna ya kuboresha ufundishaji na ufundishwaji
katika zile shule zilizopo ili wanafunzi wapate ujuzi wanaohitaji sasa na
baadaye katika maisha yao.
Ujuzi au uwezo
huu ni pamoja na ule utakaomuwezesha mwanafunzi kujiamini na kujituma, kuweza
kutatua matatizo na kukabiliana na changamoto kwa ufanisi na kuchambua na kutathmini
taarifa kwa ufasaha na umakini zaidi.
Elimu yetu
inapaswa iwape wanafunzi uwezo wa kutumia mitazamo waliyojifunza kwenye eneo
moja katika maeneo mengine pamoja na kuwapa uwezo wa kuelewa na kuwa tayari kuchangia
mahitaji ya jamii zao na taifa kwa ujumla.
Dk. Hillary
Dachi yeye alizungumzia zaidi kuporomoka kwa hadhi ya ualimu tangu nchi
ilipopata uhuru kiasi kwamba sasa hivi walimu wanaishi maisha ya dhiki na wengi
hawaipendi kazi hiyo.
Dk. Dachi anaona
kuwa taifa halitapata waalimu wa kutosha ikiwa hakuna juhudi za makusudi za
kumfanya mwalimu aliyepo aendelee kufanya kazi yake kwani kwa sasa wengi
hukimbia taaluma zao za ualimu na kuhamia katika taaluma zingine.
Kukosekana kwa
Bodi ya taaluma ya ualimu ambayo ingeweza kusajili walimu na kusimamia maadili
na mambo mengine yanayohusiana na taaluma ya ualimu. Hatuna vyama vya kitaaluma
vya walimu. Mfano zamani kilikuwepo chama kinaitwa Chama cha Kitaalamu cha
Walimu Tanzania yaani (CHAKWATA)
Ualimu umepoteza
hadhi na heshima yake katika jamii. Ni kazi ambayo kwa vijana wengi ni chaguo
lao la mwisho.Mfano imezoeleka sana nchini kwa mtoto asipo-fanya vizuri. Kwa
maneno mengine akifeli akapata madaraja ya chini sana tunasema mtafutie angalau
kozi ya ualimu.
Wakimkuta pale
nyumbani ukasema bado nahangaika unajua hakufanya vizuri wanasema ina maana umekosa
hata kozi ya ualimu? Hata ualimu umekushinda? Hali hii inasikitisha sana.
Walio wengi,
taaluma ya ualimu ni kama suluhisho la maisha kwamba unapokosa kila kitu,
anakuwa hana jinsi ila ni kukimbilia kujifunza ualimu.
Na kwa sababu
ukiwa katika ualimu ni rahisi sana kujiendeleza, kwa hiyo walio wengi
wanabadilisha taaluma wanaenda katika taaluma nyingine.
Hali hii
inasababisha ugumu wa kupata walimu wa kutosheleza kwa sababu hakuna namna
yeyote tunayoifanya kama serikali kuhakiki-sha kwamba walimu wanaipenda kazi
yao, wanaendelea kufundisha na wanapenda kufahamika kama walimu.
Ifike mahala
sasa serikali ifanyie kazi changamoto hizi badala ya kuhangaika kubadilisha
madaraja wakizani kuwa ndiyo suluhisho la kuporomoka kwa ubora wa elimu
Tanzania.
Yapo mengi ya
kueleza ila haya niliyoeleza yanatosha kuwa kianzio tosha kwa waliopewa dhamana
ya kusimamia elimu nchini,wadau wa elimu na watanzania kwa ujumla kushikamana
na kila mmoja kuwajibika katika nafasi yake ili kuinusuru elimu yetu kwa
mustakabali wa vizazi vyetu naTaifa kwa ujumla.
By
Undergraduate at
Tumaini University Dar es salaam.
0 comments:
Post a Comment