MAWAZIRI WATEULE WAREJESHE IMANI YA WATANZANIA DHIDI YA SERIKALI
Siku chache tu zimepita tangu kuenguliwa kwa mawaziri wanne wa serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania  kutokana na kushindwa kuisimamia vyema  watendaji katika operesheni tokomeza ujangili hali iliyopalekea ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu ikiwemo mauaji pamoja na udharilishaji wa kijinsia uliosadikika kufanywa na watendaji wa operesheni hiyo.

Mawaziri ambao Rais alitengua kuendelea kusimamia wizara zao ni pamoja na  aliyekuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo, bwana David Mathayo, aliyekuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, bwana Shamsi Vuai Nahodha, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, bwana Emmanuel Nchimbi na aliyekuwa Waziri wa Mali asili na Utalii, Balozi Hamisi Kagasheki.

Hata hivyo, uamuzi wa Rais kuwaondoa mawaziri hao wanne hautakuwa na tija kama hawataondolewa pia viongozi wa Vyombo vya Dola ambavyo vimelaumiwa na wabunge kwa kuhusishwa na uvunjaji wa haki za binadamu uliojitokeza katika operesheni tokomeza ujangili.

Serikali pia inapaswa kuwashughulikia Makatibu Wakuu wote na wakurugenzi wao wa Wizara nne husika, pamoja na ile inayosimamia Utawala Bora, Wizara ambayo pia inasimamia Usalama wa Taifa kwai wao pia ni sababu kubwa ya madhra yaliojitokeza kwenye operesheni tokomeza ujangili.

Hata hivyo serikali pia inapaswa kuchunguza kwa kina yale ambayo yamekuwa yakiendelea, hususan katika Wizara ya Mali asili na Utalii, hasa katika eneo la vitalu vya uwindaji na kadhalika. Kumekuwa na madai lukuki ya rushwa katika eneo hili!

Serikali ya Raisi Kikwete imaevunja rekodi yakufanyika kwa mabadiliko ya mara kwa mara kwenye baraza la mawaziri kutokana na uwepo wa watendaji wasiowajibika hali inayopelekea hasara pamoja na maafa kwa Taifa .
Ikumbukwe mabadiliko ya baraza la mawaziri yalianza mwaka 2008 baada ya kuvujwa kwa baraza la mawaziri kutokana na kujiudhuru kwa aliyekuwa waziri mkuu bwana Edward Lowasa kulikosababishwa na kashfa ya Richmond kulikofuatiwa na kujiuzuru kwa aliyekuwa waziri wa nishati na madini  Dk.Ibrahim Msabaha kutokana na kashfa ya Richmond .
mabadilko mengine ni Nazri Karamagi alingolewa kashfa ya Buzwagi,Ezekiel Maige alingolewa kashfa ya twiga,Mustafa Mkulo wa wizara ya fedha aling’olewa kashfa ya kiwanja,Dk.Haji Mponda alingolewa mgomo wa madaktari,William Ngeleja alienguliwa kashfa ya umeme pamoja na mabadiliko megine mengi.

Kitendo cha Raisi kuwavua  nyadhifa mawaziri hao kimesaidia kuiokoa serikali yake dhidi ya kupigiwa kura na wabunge ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu wake hatua ambayo ingempelekea Rais  kuvunja serikali yake au yeye mwenyewe kupigiwa kura hiyo na hivyo kulipeleka taifa katika uchaguzi mkuu wa kuchagua serikali nyingine.

Aidha baada ya kueguliwa kwa  mawaziri  hao wanne watanzania wanasubiri kwa hamu wateule wapya wa nafasi zilizowazi kwa imani ya kuwa wateule hao watakwenda kusafisha uozo ulioko kwenye wizara hizo kwa kuwawajibisha watendaji mizigo,wabadhilifu na wabinafsi ndani ya wizara hizo na kurudisha heshima na imani ya watanzania iliyotoweka kwa sasa.

Watanzania pia wanategemea kuona watendaji waliosababisha madhara kwa kukiuka haki za kibinadamu vikiwemo vyombo vya dora wanashuhurikiwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi na si kuishiakuvuliwa nyadhifa kwa mawaziri.

Naamini imani ya watanzania dhidi ya baadhi ya watendaji wa serikali itarejea pindi hatua za makusudi dhidi ya watendaji wadhembe zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kuwafukuza kazi na kuwachukulia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwashtaki ili iwe funzo kwa wengine katika utendaji wao.

0 comments:

 
Top